• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • JPM ataka Ma-RC kukuza viwanda

    (GMT+08:00) 2017-06-14 20:19:52

    RAIS John Magufuli akiongoza kikao na wakuu wa mikoa yote pamoja na baadhi ya mawaziri amewaagiza wakuu wa mikoa Tanzania Bara, kusimamia kwa ukaribu utekelezaji wa mpango wa ujenzi wa viwanda katika maeneo yao ili kuwawezesha wananchi kuongeza thamani ya mazao yao na kuzalisha ajira.

    Aidha anasema kuwa kila mkuu wa mkoa anapaswa kufanyia kazi fursa za uanzishaji wa viwanda katika eneo lake na kuhakikisha anashawishi wawekezaji, kutumia fursa hizo kama inavyofanyika katika mkoa wa Pwani, ambako tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani, viwanda vikubwa 83 vimejengwa na vingine kukamilika huku viwanda vidogo zaidi ya 120 pia vikiwa vimejengwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako