• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mwili wa Cheick Tiote wasafirishwa Ivory Coast

    (GMT+08:00) 2017-06-15 09:11:55

    Jumatatu ya wiki iliyopita ulimwengu wa soka hususan barani Afrika ulipokea taarifa za kushtusha kuhusiana na kifo cha kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast aliyekuwa anaichezea Beijing Enterprises ya Beijing China.

    Tiote aliyewahi kuichezea timu ya Newcastle United ya England alifariki ghafla mazoezini akiwa na timu yake ya Beijing, na mwili wake jana uliagwa na wachezaji wenzake wa hapa Beijing na hatimaye kusafirishwa hadi kwao Ivory Coast. Cheick Tiote alikuwa miongoni mwa wachezaji wa Ivory Coast waliotwaa Kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2015, Tiote hadi anapoteza maisha alikuwa kacheza jumla ya mechi 246 ngazi ya klabu huku timu ya taifa ya Ivory Coast ameichezea michezo 52.

    Cheick Ismael Tiote alijiunga na Being Enteprises mwaka huu wa 2017 .

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako