Wenyeji Russia wameanza vyema katika mechi ya kundi A ambayo ni mechi ya ufunguzi ya FIFA kombe la mabara (FIFA Confideration Cup) iliyfanyika juzi, mashindano ambayo huandaliwa na FIFA mwaka mmoja kabla ya fainali za kombe la dunia kwenye nchi ambayo ndiyo mwenyeji wa fainali hizo. Russia wameichapa New Zealand mabao 2-0.
Mechi zingine ziliendelea jana katika kundi A, Ureno yalazimishwa sare na Mexico ya 2-2. Katika kundi C, Cameroon wameanza vibaya kwa kukubali kipigo cha 2-0 toka kwa Chile.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |