Mkutano na waandishi wa habari wa maonesho ya kwanza ya filamu ya kimataifa ya China na Afrika yaliyoanzishwa na Radio China Kimataifa CRI na chuo kikuu cha filamu cha Beijing na kuendeshwa na kampuni ya Global Max Media Group umefanyika jana mjini Shanghai.
Mkutano huo ulitangaza kuwa maonesho ya kimataifa ya filamu ya China na Afrika yatafanyika huko Capetown nchini Afrika Kusini kuanzia tarehe 12 hadi tarehe 22 mwezi Oktoba mwaka huu.
Akizungumza kwenye mkutano huo, naibu mhariri mkuu wa Radio China Kimtaifa Bw. Ren Qian amesema Radio China Kimataifa itafanya juhudi kuhimiza mawasiliano kati ya filamu za China na za Afrika kwenye msingi wa kuanzisha maonesho ya kimataifa ya filamu ya China na Afrika, na kuinua kiwango cha mawasiliano ya utamaduni wa filamu kati ya pande hizo mbili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |