Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang amekutana na wajumbe wa Marekani na China wanaohudhuria mazungumzo ya 9 ya viongozi wa wanaviwanda na wafanyabiashara yanayofanyika leo asubuhi hapa Beijing.
Bw. Li amesema ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara ni msingi muhimu wa uhusiano kati ya China na Marekani. China inayakaribisha makampuni ya nchi mbalimbali ikiwemo Marekani kuanzisha shughuli hapa China, ili kunufaishana na kutimiza mafanikio ya pamoja
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |