Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB imezindua mkakati unaolenga kufungua nafasi milioni 25 za ajira kwa vijana barani Afrika ndani ya miaka kumi ijayo.
Mpango huo wa kati ya mwaka 2016 na 2025 unaangazia utengamano, uvumbuzi na uwekezaji kwenye maeneo muhimu.
Rais wa benki hiyo Akinwumi Adesina amesema watalenga kufadhili miradi kama vile kilimo n kawi ili kuwaingiza vijana wengi katika ajira.
Aidha benki hiyo itawasaidia na sera bora za kujihusisha na biashara kikanda na kimataifa.
Tayari uwekezaji wa benki hiyo umefikia dola bilioni 10 katika mwaka wa 2016 ikiwekeza hasa kwenye miradi ya miundo mbinu ya uchukuzi na kawi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |