Umoja wa Mataifa umekadiria kuwa idadi ya watu duniani inatarajiwa kuwa bilioni 8.6 mwaka 2030, na kufikia bilioni 9.8 ifikapo mwaka 2050, licha ya kiwango cha uzazi kuwa chini kote duniani. Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema kwa sasa idadi ya watu duniani ni bilioni 7.6, na imeongezeka kutoka bilioni 7.4 ya mwaka jana kutokana na kiwango cha juu cha uzazi katika nchi zinazoendelea, lakini idadi ya watoto kote duniani imeendelea kupungua.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |