Serikali ya China imetoa mifuko laki moja ya chakula cha msaada kwa ajili ya watu wa Kenya walioathiriwa na ukame. Akiongea kwenye hafla ya kukabidhi msaada huo, balozi wa China nchini Kenya Bw Liu Xianfa amesema mchele huo ni sehemu ya mifuko laki 4.5 iliyoahidiwa na serikali ya China.
Msaada huo umetolewa wakati kwa mara ya kwanza ubalozi wa China nchini Kenya umetoa ripoti, kuhusu michango ya maendeleo inayotolewa na mashirika ya China nchini Kenya. Mashirika mbalimbali yanayohusu ujenzi, elimu, teknolojia, usafirishaji yametoa ripoti kuhusu jinsi wakenya wanavyonufaika na uwepo wao nchini Kenya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |