Shirika la ndege la Rwanda, RwandAir litaanza safari za moja kwa moja kutoka Kigali hadi Brussels Ubelgiji kuanzia mwezi Julai.
Shirika hilo limesema kupitia kwa taarifa yake kwamba litatumia ndege yake aina ya Airbus A330 na litafanya ziara mara tatu kwa wiki lakini itasimama London kwenye safari ya kurejea kutoka Brussels.
Kaimu mkurungezi wa Rwandair Chance Ndagano, amesema safari hiyo mpya ni sehemu ya mipango yake ya upanuzi na inafikisha 23 maeneo linakohudumu shirika hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |