Rais Paul Kagame wa Rwanda amewasilisha formu kwa tume ya uchaguzi ya taifa NEC na kujiandaa kugombea urais kwa muhula wa tatu.
Rwanda itafanya uchaguzi wa urais Agosti 4 kwa mara ya tatu tangu mwisho wa serikali ya mauaji ya halaiki mwaka 1994.
Tume ya uchaguzi ya Rwanda inatarajiwa kupitia na kukubali wagombea kabla ya kutoa orodha ya muda ya wagombea wanaostahiki Juni 27. Majina ya wagombea rasmi yatatangazwa Julai 7, wiki moja kabla ya kampeni kuanza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |