Gilles Muller kutoka Luxembourg amemuondoa Mfaransa Jo-Wilfried Tsonga kwenye michuano ya Aegon, inayoendelea nchini England.
Muller ambaye hana jina kubwa katika ramani ya mchezo wa tenesi alimfunga Tsonga kwa seti mbili katika raundi ya pili ya mchuano wao.
Katika seti ya kwanza Muller alishinda kwa 6-4 na seti ya pili akishinda kwa 6-4.
Tsonga anakua nyota wa nne kutupwa nje ya mashindano hayo baada ya Andy Murray, Stan Wawrinka na Milos Raonic kuondolewa hapo siku ya Jumanne .
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |