Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amemteua Bw. Ghassan Salame kutoka Lebanon kuwa mjumbe wake maalum wa suala la Libya, na kiongozi wa tume ya Umoja wa Mataifa nchini Libya.
Bw. Ghassan Salame aliwahi kuwa profesa wa uhusiano wa kimataifa katika Chuo cha siasa cha Paris kwa muda mrefu, pia alikuwa mshauri mwandamizi wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, na mshauri wa mambo ya siasa wa tume ya Umoja wa Mataifa nchini Libya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |