Bunge la Somalia limepitisha kwa kauli moja muswada wa Sheria ya Taifa ya Mawasiliano ambao unatarajiwa kurekebisha sekta ya mawasiliano ya simu nchini humo.
Muswada huo uliowasilishwa na waziri wa Posta, Simu na Teknolojia Abdi Ashur Hassan, ni moja ya miswada ya muda mrefu ambayo ilikuwa bado haijapitishwa na bunge. Waziri huyo amesema, mara baada ya muswada huo kusainiwa, utafanya marekebisho kwenye sekta ya mawasiliano ya simu, ambayo moja ya sekta zinazokua kwa kasi nchini Somalia, na kulinda haki za mtumiaji na mwekezaji.
Waziri huyo amesema, muswada huo ulikuwa moja ya vipaumbele vya uongozi mpya wa wizara yake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |