Waziri mkuu wa Tanzania Bw Kassim Majaliwa amewataka maofisa wa Mamlaka ya Kodi ya Mapato Tanzania (TRA) wakusanye kodi za majengo kwa kuzingatia sheria na wasitoze kodi ya majengo ya wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60. Waziri Mkuu amewataka moafisa hao wakusanye kodi ya majengo kwenye maeneo ya mjini na siyo vijijini kwani kodi hiyo haiwahusu.Wakati huo huo Bwana Majaliwa pia amewataka wananchi wanaonunua bidhaa kudai risiti lakini wahakikishe wanapewa risiti yenye kiwango halisi walicholipia ili kuzuia ukwepaji wa kodi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |