Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa jana alitoa taarifa kwa kupitia msemaji wake akitoa salamu za pole kwa watu na serikali ya China kutokana na vifo na majeruhi ya watu katika tukio la maporomoko ya maji na mawe lililotokea mkoani Sichuan.
Taarifa hiyo imesema Bw. Guterres anawatakia watu waliojeruhiwa kupona mapema. Kama iko haja Umoja wa Mataifa utapenda kutoa misaada kwa China kadiri iwezekanavyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |