Dereva Lewis Hamilton amesema kitendo cha dereva mwenzake Sebastian Vettel kumgonga wakati wa mbio za Azerbaijan Grand Prix ni cha aibu na hakipaswi kufanywa na dereva makini.
Madereva hao wawili waligongana wakati mbio hizo zikikaribia mwisho baada ya Vettel kuvamia nyuma ya gari la Hamilton na kisha wote wawili kupoteza muelekeo.
Vetel anasema Hamilton alishika breki kwa maksudi ili kumjaribu. Hamilton akapinga hilo na kusema kitendo hicho sio cha kimichezo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |