Mahakama kuu ya Marekani imeamua kuruhusu utekelezaji wa sehemu ya zuio la uhamiaji lililotolewa na serikali ya Donald Trump na kusema itaanza rasmi kujadili uhalali wa zuio hilo mwezi Oktoba mwaka huu. Taarifa ya kisheria iliyotolewa na mahakama hiyo inasema zuio la uhamiaji haliruhusiwi kuwazuia watu wenye uhusiano halisi na watu binafsi na mashirika ya Marekani kuingia nchini humo, lakini linaruhusiwa kuzuia watu ambao hawajawahi kuingia Marekani, hawana ndugu wala hawana uhusiano wowote nchini Marekani, wasiingie nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |