• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya:Maduka ya jumla ya Nakumatt yaendelea kusambaratika

    (GMT+08:00) 2017-06-27 19:09:13

    Tangu kuanzishwa kwake mnamo 1987, kampuni hii inayomiliki maduka kadha nchini, imefurahia uthabiti na ufanisi mkubwa kibiashara.

    Lakini uthabiti huo haupo tena kwani kufikia sasa Nakumatt inazongwa na mzigo wa madeni ya kima cha Sh15 bilioni, hali ambayo imelazimu kufungwa kwa baadhi ya matawi yake. Mfano ni kufungwa kwa tawi la barabara ya Ronald Ngala mwezi Februari mwaka huu.

    Mwenendo wa baadhi ya wafanyakazi kushirikiana na wawasilishaji bidhaa kulipia bidhaa ambazo hazijawasilishwa, umetajwa kuwa mojawapo ya shida kubwa inayokumba Nakumatt.

    Aidha, inadaiwa kuwa wakati mwingine wafanyakazi wa duka hili huagiza bidhaa ambazo hazinunuliwi kwa haraka.

    Hali hiyo imewafanya maelfu ya wateja katika matawi yake 66 nchini Kenya, Uganda na Rwanda kukumbwa na uhaba wa bidhaa muhimu katika maduka hayo huku wafanyakazi wakiachishwa kazi.

    Vile vile, kulingana na Shah, Halmashauri ya Ukusanyaji Ushuru (KRA) ilitoza Nakumatt faini ya Sh1 bilioni ambayo iliathiri shughuli za kampuni hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako