Mkutano wa saba wa Baraza la China na Ulaya ulifanyika jana kwenye makao makuu ya Umoja wa Ulaya mjini Brussels. Maofisa, wataalamu na wasomi kutoka China na Ulaya wamejadili kwa kina masuala yanayoyafuatiliwa kwa pamoja, ikiwemo pendekezo la "Ukanda mmoja na Njia moja", chini ya kaulimbiu ya "Ushirikiano kati ya China na Ulaya katika zama ya sintofahamu". Kiongozi wa ujumbe wa China katika Umoja wa Ulaya Yang Yanyi .amesema China na Ulaya zina wajibu na fursa kubwa ya kuendeleza ushirikiano kati yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |