• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Scotland yasema haitapiga kura za maoni kuhusu kujitenga na Uingereza kabla ya Brexit

    (GMT+08:00) 2017-06-28 09:27:38

    Waziri mkuu wa serikali ya Scotland na kiongozi wa chama tawala cha SNP Bibi Nicola Sturgeon, amesema serikali ya Scotland itapanga upya ajenda ya kupiga kura za pili za maoni kuhusu kujitenga na Uingereza, na haitapiga kura hizo kabla ya Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya.

    Bibi Sturgeon amesema, matokeo ya uchaguzi mkuu wa Uingereza yameonesha udhaifu wa serikali ya Uingereza, hali ambayo inaweza kuifanya serikali ya Uingereza ilegeze msimamo kwenye mazungumzo ya kujitoa Umoja wa Ulaya, na pia imepunguza uwezekano kwa Uingereza kubaki kwenye soko la pamoja la Ulaya.

    Ameongeza kuwa serikali ya Scotland itaweka upya mpango wa kupiga kura za maoni kuhusu kujitenga na Uingereza, kwa kuzingatia mambo ya kujitoa Umoja wa Ulaya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako