Soko la Pamoja la Nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) limehimiza wanachama wake kuwekeza zaidi katika utafiti na miradi ya ubunifu ili kuharakisha maendeleo ya kiuchumi katika kanda.
Akizungumza wakati wa mkutano wa tatu wa mwaka wa Utafiti wa COMESA Mjini Kigali, Dr Kipyego Cheluget, Katibu Mkuu wa COMESA, amesema changamoto za kiuchumi ambazo zinakabiliwa na Afrika na kanda ya COMESA,zinaweza kushughulikiwa vizuri kupitia sera za msingi.
Mkutano huu wa siku tano unaangalia kuimarisha ushiriki wa serikali na wadau wengine muhimu katika ajenda ya ushirikiano wa kikanda kwa kushirikiana na Kujadili matokeo ya utafiti.
Akizungumza katika mkutano huo, Robert Opirah, mkurugenzi mkuu wa biashara na uwekezaji katika Wizara ya Biashara, Viwanda na Masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, ameonya kuwa ahadi zilizofanywa na wanachama wa COMESA kutekeleza mipango ya ushirikiano wa kikanda inaweza kupitwa na matukio, ikiwa si ya haraka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |