Rwanda inatarajia hivi karibuni kuzindua mamlaka ya Ukaguzi, ushindani na ulindaji wa wateja kufuatia kupitishwa kwa mswada bungeni wa kuwa na mamlaka hiyo.
Kutokuwepo kwa mamlaka hiyo kumesababisha athari mbaya kutokana na kuwepo kwa wafanyabiashara wanaowapunja wateja.
Mtafiti kwenye taasisi ya sheria na maendeleo Daniel Ndayisaba amesema Rwanda ilikuwa haina njia ya kutambua iwapo makampuni au wafanyabiashara wanaendesha ushindani usiokuwa halali.
Majukumu ya mamlaka hiyo yatakuwa ni kukagua ubora wa bidhaa zikiwemo kemikali za kilimo na bidhaa za mifugo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |