• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda: Wachimba madini eneo la Mubende Uganda wahofia watafurushwa

    (GMT+08:00) 2017-06-29 19:22:05

    Wachimba madini wadogo wadogo katika eneo la Mubende nchini Uganda wamemuomba rais Yoweri Museveni kuwasaidia ili wasifurushwe kutoka eneo lao la kuchimba.

    Maelfu ya wachimbaji wako kwenye eneo la kilomita tano mraba lakini wanahofia watafurushwa ili eneo hilo litumike kuchimba dhahabu na kampuni kubwa.

    Mwenyekiti wao John Bosco Bukya, amesema ikiwa wataondolewa basi zaidi ya watu 25,000 watakosa ajira,

    Tarehe 13 mwezi huu agizo la kuwafurusha wachimbaji hao lilitolewa baada ya mkutano kati ya Rais Museveni na wasimamizi wa kampuni ya

    Gemstone International lakini sasa wanasema rais hakushauriwa vizuri kuhusu hatua ya kutaka kuwafurusha.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako