Waziri mkuu wa Russia Bw. Dmitry Medvedev amesema serikali ya Russia inapanga kuongezea muda hatua za kupambana na vikwazo ilivyowekewa na Umoja wa Ulaya hadi kufikia mwishoni mwa mwaka kesho, ili kujibu hatua ya Umoja wa Ulaya kuongeza muda wa vikwazo dhidi ya Russia. Jumatano wiki hii Baraza la Umoja wa Ulaya lilitoa taarifa likitangaza uamuzi wa kurefusha tena muda wa vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Russia hadi mwishoni mwa mwaka kesho, kutokana na utekelezaji usio wa kuridhisha wa makubaliano ya Minsk.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |