Mapigano makali yametokea kati ya polisi na watu walioshambulia kituo cha polisi huko Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC, na kusababisha vifo na majeruhi ya watu kadhaa huku baadhi ya wafungwa wakitoroka.
Wizara ya mambo ya ndani ya DRC imetoa taarifa ikisema, shambulizi hilo limefanywa na kundi la watu wasiojulikana.
Msemaji wa polisi nchini humo amesema, hivi sasa hali imedhibitiwa, na kwamba mshambuliaji mmoja aliuawa kwenye mapigano na wengine watatu wamekamatwa, huku askari wanne wakijeruhiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |