Bibi Lam Cheng Yuet-ngor ameapishwa kuwa mkuu wa mkoa wa utawala maalumu wa Hong Kong, kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Hong Kong kurudi kwa China iliyofanyika leo asubuhi huko Hong Kong, ambapo rais Xi Jinping wa China amehudhuria na kusimamia hafla hiyo.
Baraza la serikali ya awamu ya 5 ya mkoa wa utawala maalumu wa Hong Kong pia limeapishwa chini ya usimamizi wa rais Xi, na baraza la utekelezaji la mkoa huo kuapishwa na Bibi Lam.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |