Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limetoa taarifa ya mwenyekiti likiipongeza tume ya umoja huo nchini Cote d'Ivoir UNOCI ambayo imemaliza jukumu tarehe 20 Juni kwa juhudi ilizofanya katika miaka 13 iliyopita.
Baraza hilo limesema limefurahia maendeleo makubwa yaliyopatikana nchini humo katika kuimarisha amani, utulivu na ustawi wa uchumi. Baada ya UNOCI kuondoka, Cote d'Ivoire inatakiwa kuendelea kufanya juhudi katika kuwaadhibu wahalifu, kusukuma mbele mapatano ya kitaifa na muungano wa kijamii, kufanya mageuzi katika idara za usalama, na kuwasaidia wanawake kushiriki kwenye mambo ya siasa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |