Kamati ya Umoja wa Ulaya tarehe 1 mwezi Julai ilirefusha hatua ya uungaji mkono kwa wakulima wa matunda wa Ulaya kwa mwaka mmoja ili kupunguza hasara za wakulima hao kutokana na amri ya Russia kuhusu kupiga marufuku uagizaji wa mazao ya kilimo kutoka nchi za magharibi.
Tovuti ya kamati ya Umoja wa Ulaya ilitoa ripoti ikisema hatua hiyo itakayotekelezwa mpaka mwishoni mwa mwezi Juni mwaka 2018 itatoa EURO milioni 70 kwa wakulima wa matunda wa nchi 12 wanachama wa Umoja wa Ulaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |