Rais Xi Jinping amewasili Moscow, Russia na kuanza ziara ya kiserikali nchini humo. Rais Xi amesema China na Russia ni majirani, marafiki na wenzi wema. Anatarajia katika ziara hiyo atabadilishana maoni kwa kina na rais Vladmir Putin kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya pande mbili, masuala makubwa ya kimataifa na kikanda, na kusukuma mbele uhusiano wa wenzi wa kimkakati katika pande zote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |