Timu za JKU Academy zimeondoka jana kuelekea Arusha kwenye mashindano ya vijana ya Afrika Mashariki na kati (Rolling Stone) yanyotarajiwa kuanza rasmi Julai 9 hadi 19 mwaka huu.
JKU mwaka huu wanatarajia kushiriki timu tatu tofauti ikiwemo timu ya wachezaji wenye umri wa chini ya miaka 13, 15 na 17.
Mashindano hayo yamepangwa kufanyika katika vituo tofauti vya Arusha na Manyara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |