Thika Queen bado inaendelea kujikita kileleni mwa ligi kuu ya soka ya wanawake kanda A baada ya kuwafunga Mombasa Olympic goli 2-1 katika mechi iliyochezwa uwanja wa KPA Mbaraki Sports Club mjini Mombasa.
Kwingineko mechi nyingine ya kundi A iliyokuwa iwakutanishe wenyeji Spedag na wageni soccer sisters haikuchezwa kwenye uwanja wa shule ya msingi Ronald Ngala baada ya wageni kukataa kucheza wakidai uwanja hauko katika kiwango cha kuchezewa soka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |