Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) leo kitavaana na timu ya Taifa ya Zambia, Chipolopolo katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya kombe la COSAFA, huku kikosi hicho kikiongezewa nguvu na mshambuliaji John Bocco.
Meneja wa Taifa Stars Danny Msangi amesema wamejiandaa vizuri kukabiliana na Chipolopolo, na John Bocco amechukua nafasi ya mshambuliaji Mbarak Yusuph ambaye ni majeruhi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |