Mkutano wa 29 wa kilele wa Umoja wa Afrika uliofanyika kwenye makao makuu ya Umoja wa Afrika huko Addis Ababa, umesema utaimarisha ushirikiano wa kikanda na wa kimataifa ili kukabiliana na changamoto ya usalama kwa pamoja.
Kutokana na hali ngumu ya usalama barani Afrika, amani na usalama ilikuwa ajenda muhimu ya mkutano huo. Mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Afrika Bw. Moussa Faki alisema, amani na usalama ni msingi wa maendeleo ya uchumi wa nchi za Afrika, na suala la amani na usalama pia ni changamoto kubwa kabisa inayoukabili Umoja wa Afrika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |