Msaidizi wa rais wa Russia Bw Ushakov ametangaza kuwa rais Vladmir Putin atakutana na mwenzake wa Marekani Donald Trump kwa mara ya kwanza tarehe 7 mwezi huu.
Bw Ushakov amesema rais Putin na rais Trump watakutana tarehe 7 kando ya mkutano wa kilele wa nchi za Kundi la G20 utakaofanyika mjini Hamburg, Ujerumani. .
Habari zinasema viongozi hao watajadiliana masuala ya Syria, Ukraine pamoja na mapambano dhidi ya ugaidi wa kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |