Watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa kundi la Al Shabaab la Somalia wamevamia kituo cha polisi katika mji wa pwani wa Lamu kaskazini mwa Kenya leo asubuhi na kuharibu mnara wa mawasiliano katika eneo hilo.
Kamishna wa Kaunti ya Lamu Joseph Kanyiri amethibitisha tukio hilo, na kusema wapiganaji hao walivamia kijiji kimoja kwenye kaunti hiyo na kuharibu mnara wa simu wa kampuni ya Safaricom, hivyo kuvuruga mawasiliano katika eneo hilo.
Kamanda wa polisi kanda ya pwani Philip Tuimur amesema, vikosi vya usalama viliwasili haraka kwenye eneo la tukio na kukabiliana na washambuliaji hao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |