Idadi ya Wakenya ambao waliwasilisha fomu za kuonyesha malipo ya ushuru yao mwishoni mwa mwezi Juni iliongezeka kwa asilimia 54.
Lakini zaidi ya wafanyikazi na wafanyibiashara milioni 2.4. wanahofu ya kulipa faini ya sh 20,000 kwa kutofuata maagizo.
Mamlaka ya Mapato ya Kenya (KRA) imesema uwasilishaji wa fomu ulizidi lengo lao la milioni 2.
Karibu Wakenya milioni 1.579 waliwasilisha fomu zao za kuonyesha malipo ya ushuru mwaka jana.
KRA ilikusanya ushuru wa sh bilioni 217.75 (PAYE) kinyume na lengo lake la Sh bilioni 251.98.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |