Hazina ya malipo ya uzeeni nchini Uganda (NSSF) imekusanya hadi shilingi bilioni 100 kutoka kwa wanachama wake mwezi Juni.
Mkurungezi wa hazina hiyo Richard Byarugaba amesema makusanyo hayo ni afueni kubwa kwani walikuwa na fedha ndogo kipindi sawa na hicho mwaka jana.
Hii ni mara ya kwanza kwa NSSF kufikisha shiligi bilioni 100 ndani ya mwezi mmoja.
Mwaka jana mwezi juni hazina hiyo ilipata shilingi bilioni 85.
Kwa mwezi NSSF inalenga kukusanya shilingi bilioni 77 .
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |