Kamati ya Umoja wa Ulaya huko Brussles ilitoa taarifa ikisema kuwa Umoja wa Ulaya na Canada zilikubaliana kutekeleza makubaliano ya biashara huria kwa muda kuanzia Septemba 21 na kuondoa wingi wa ushuru.
Taarifa hiyo imesema kuwa mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Ulaya Bw. Jean-Claude Juncker na waziri mkuu wa Canada Bw. Justin Trudeau siku hiyo walifanya mazungumzo huko Hamburg nchini Ujerumani, ziliweka uamuzi huo ili kuhimiza kazi zote zimalizike kabla ya tarehe hiyo ya mwisho.
Taarifa hiyo imesema kuwa hatua ijayo ni kuyahimiza mashirika ya utungaji sheria kuidhinisha makubaliano hayo. Baada ya kuidhinishwa na mabunge yote ya nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya, makubaliano hayo yatatekelezwa kihalisi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |