Rais Donald Trump amekutana na mwenzake wa Russia Vladimir Putin kando ya mkutano wa wakuu wa kundi la G20 uliofanyika Hamburg, Ujerumani.
Baada ya mkutano huo, waziri wa mambo ya nje wa Russia Bw Sergey Lavrov amesema rais Trump amekubali kauli ya Rais Putin kuhusu Russia kutoingilia uchaguzi mkuu wa Marekani. Rais Putin amesema amejibu maswali ya Rais Donald Trump ambaye ameridhishwa na majibu yake.
Rais Trump amesema amejadiliana na Rais Putin na kupanga kuweka mfumo wa kulinda usalama wa mtandao wa internet ili kuzuia mambo yanayoharibu usalama wa taifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |