Burundi inaendelea kushuhudia wimbi la wakimbizi kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo. Mamia ya wakimbizi wamekuwa wanavuka mpaka na kuingia Burundi wakikimbia mapigano yanayotokea katika eneo la mashariki mwa DRC. Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa mataifa UNHCR linakadiria kuwa Burundi imewapa hifadhi raia zaidi ya elfu 58 kutoka DRC.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |