Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki atafanya ziara nchini Qatar, Kuwait na Saudi Arabia, na kuzishawishi nchi zinazohusika kutatua mgogoro wa kukata uhusiano wa kibalozi kwa njia ya mazungumzo.
Gazeti moja la nchini Uturuki limeandika kuwa, rais Erdogan akiwa njiani kurejea Uturuki baada ya kuhudhuria mkutano wa kilele wa kundi la nchi 20 huko Hamburg Ujerumani, amesema huenda atafanya ziara kwenye nchi hizo tatu baada ya tarehe 15 mwezi huu, na anataka kuzihimiza nchi husika kufanya mazungumzo tena.
Rais Erdogan amesema Uturuki inaziunga mkono juhudi za Kuwait za kutatua mgogoro wa nchi nyingine za kiarabu kukatisha uhusiano wa kibalozi na Qatar.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |