Wawakilishi kutoka sekta ya mafuta kote duniani wamekutana kwenye Mkutano wa 22 wa Baraza la mafuta duniani ulioanza Jumapili mjini Istanbul, kujadili mustakbali wa nishati katika mazingira ya ongezeko la idadi ya watu duniani kwa miongo kadhaa ijayo. Mkurugenzi mtendaji mkuu wa Kampuni ya Royal Dutch Shell Bw. Ben Van Beurden amesema idadi ya watu duniani inatarajiwa kufikia bilioni 11.2 ifikapo mwaka 2100, na Afrika pekee itachangia ongezeko la watu bilioni 3.2, na hivyo kuongeza kwa kiasi kikubwa mahitaji ya nishati duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |