Rais Petro Poroshenko wa Ukraine amesema nchi yake bado haina mpango wa kuwasilisha ombi la kujiunga na Jumuiya ya kujihami ya nchi za magharibi NATO. Kwenye mkutano wa kamati kati ya Ukraine na NATO uliofanyika jana huko Kiev, rais Poroshenko amesema kipaumbele cha Ukraine kwa sasa ni kuimarisha ushirikiano na NATO kwenye mageuzi ya sekta za ulinzi na usalama, ili kuziboresha na kufikia vigezo vya NATO.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |