• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Nyota wa soka wa England Wayne Rooney, amesema anasubiri kwa hamu sana kuzuru Tanzania.

    (GMT+08:00) 2017-07-11 10:10:57
    Mshambulizi matata wa zamani wa timu ya Manchester United ya Uingereza Wayne Rooney atakuwa kwenye kikosi cha Everton kitakachocheza mechi ya kujiandaa kwa msimu ujao utakaofanyika Tanzania baadaye wiki hii.

    Rooney, amesema ziara hiyo itampa fursa mwafaka ya kufahamiana na wachezaji wenzake wapya.

    Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 31, anayeongoza kwa ufungaji mabao England alitia saini mkataba wa miaka miwili Goodison Park Jumapili, na kurejea kwenye klabu hiyo ambayo aliichezea akiwa na umri mdogo kabla ya kukigura na kujiunga na Manchester United.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako