• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri wa mambo ya nje wa Algeria asema kuwa wahamiaji haramu wanatishia usalama wa nchi hiyo

    (GMT+08:00) 2017-07-11 18:28:56

    Waziri wa mambo ya nje wa Algeria Bw. Abedel Kader Messahel amesema, wahamiaji haramu wanatishia usalama wa nchi hiyo, na kwamba serikali itachukua hatua za dharura kudhibiti kuingia kwa wahamiaji haramu.

    Bw. Messahel amesema hayo jana mjini Algiers alipohutubia mkutano wa kimataifa wa kupambana na ugaidi. Amesema kuwa mtandao wa makundi ya uhalifu ya kimataifa yalikusanya wahamiaji haramu na kuwaingiza nchini Algeria, na nchi hiyo imekua moja ya nchi ambazo wahamiaji haramu kutoka nchi za kusini mwa Sahara wanalenga kuhamia.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako