Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Bw. Ibrahim Ghandour ameitaka serikali ya Marekani kufanya uamuzi sahihi, na kuondoa vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Sudan.
Bw. Ghandour amesema, baada ya kuondoa vikwazo hivyo, Sudan itashirikiana na Marekani kulinda usalama wa kikanda. Timu ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan pia imetoa taarifa ikisema, katika miezi sita iliyopita, Sudan imepata maendeleo makubwa katika utoaji wa misaada ya kibinadamu. Taarifa hiyo pia imeitaka Marekani iondoe vikwazo dhidi ya Sudan haraka iwezekanavyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |