Vyombo vya habari vya Iraq vimesema, kundi la IS limetoa taarifa fupi ikithibitisha kifo cha kiongozi chake Abu Bakr al-Baghdadi na kusema kundi hilo litachagua kiongozi mpya baadaye, lakini taarifa hiyo haikueleza kwa undani kuhusu kifo cha kiongozi huyo.
Mwezi uliopita, vyombo vya habari vya Russia viliripoti kuwa al-Baghdadi huenda amefariki katika shambulizi lililofanywa na ndege za kivita za jeshi la Russia nchini Syria.
Lakini habari hiyo haikuthibitishwa na Marekani na Iraq.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |