Wanamgambo wanaoshirikiana na serikali ya maafikiano ya kitaifa ya Libya inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa, wametangaza kutwaa udhibiti wa mji wa Garabulli, kilomita 50 mashariki mwa Tripoli, baada ya mapambano makali na waasi yaliyodumu kwa siku tatu na kusababisha vifo vya watu wanne. Mapambano hayo yalitokea jumapili kati ya wanamgambo wa Brigedi ya Tripoli na waasi wanaoitii serikali iliyoondolewa ambayo inajaribu kutwaa mji mkuu Tripoli tangu mwezi Disemba mwaka 2015.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |