Jeshi la Marekani limesema bado haliwezi kuthibitisha kifo cha kiongozi mkuu wa kundi la IS Abu Bakr al-Baghdadi.
Jeshi la Marekani pia limesema, mwezi uliopita vyombo vya habari vya Russia vilitoa habari kuwa huenda al-Baghdadi aliuawa kwenye mashambulizi ya anga yaliyofanywa na jeshi la Russia nchini Syria, lakini habari lilizopata jeshi la Marekani zilionesha kuwa, Al-Baghdadi hakuuawa kwenye mashambulizi hayo.
Vyombo vya habari vya Iraq jana vilisema, kundi la IS limekiri kifo cha Bw Al-Baghdadi, na kundi hilo litachagua kiongozi mpya baadaye.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |