Mhandisi mkuu wa idara ya barabara na uchukuzi ya jimbo la Gauteng Afrika Kusini amesema ajali za barabarani zilizotokea katika mwaka wa fedha 2015/16 nchini humo zilisababisha vifo vya watu zaidi ya elfu 13 na hasara ya kiuchumi dola bilioni 10.8 za kimarekani, ikiwa ni asilimia 3.4 ya pato la taifa. Ofisa huyo amesema chanzo cha tatizo hilo ni usimamizi dhaifu wa usalama barabarani, na kukosekana kwa hatua madhubuti za kuelekeza mawasiliano barabarani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |